MATOKEO YA MRADI WA TAMPERE



MWANZA CITY COUNCIL
MWANZA-TAMPERE STRENGTHENING COOPERATION PROJECT
Tampere cultural week 29th October 2013.



Mstahiki Meya wa jiji la Mwanza,
Kaimu Mkurugenzi wa jiji la mwanza
Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Mradi,
Walimu wa shule za mradi ,
Mabibi na mabwana.
Wanafunzi wote kwa ujumla

 Awali ya yote napenda kutoa shukrani zangu kwa wageni wote waalikwa na kwa marafiki zetu kutoka Tampere Finland. Ndugu mgeni rasmi:
Mradi wa Uhusiano wa jiji la Mwanza na Tampere ni moja ya Miradi ya Halmashauri ya jiji la Mwanza hivyo ni Mradi ambao uko chini yako moja kwa moja.
Historia ya uhusiano na ndugu zetu wa Tampere una takribani miaka 22 hivi sasa, ilikuwa ni matembezi ya kawaida tu mwaka 1987 ambapo timu ya jiji la Tampere ilipokuja kutembelea hapa Mwanza wakati huo tukiwa manispaa,matembezi hayo yalipelekeea kusainiwa kwa mikataba mbalimbali,ambapo mkataba wenye mafanikio zaidi ulisainiwa mwaka 2000.
Mkataba huo uliopelekea kuanzishwa kwa mradi utaokaokuwa ukisimamia na kutekeleza shughuli mbalimbali tunakazokuwa tumekubaliana na wenzetu wa jiji la Tampere,hivyo ni dhahiri kuwa shughuli  zilizotekelezwa na zitakazo tekelezwa na Mradi huu ni  matunda ya ushirikiano kati ya jiji la Mwanza na jiji la Tampere la nchini Finland.
Baadhi ya shughuli amabazo zimeshatekelezwa na zinazoendelea kutekelezwa ni  kujengea uwezo mkubwa kikosi chetu cha zimamoto kwa kukipatia mafunzo ndani na nje ya nchi pamoja na vifaa kama vitendea kazi ,tumeweza kuotesha miti mingi sana na kuisambaza sehemu mbalimbali ya jiji letu na tumeweza kutoa mafunzo kwa waheshimiwa madiwani na watumishi wa halmashauri ya jiji letu,haya ni baadhi tu ya matunda tuliyoweza kuayapata kupitia uhusiano na wenzetu wa jiji la Tampere.

Ndugu wageni waalikwa na wadau wote wa mradi na wananchi wa mwanza kwa ujumla, Leo tunasherehekea Wiki ya Tampere jijini mwanza na wenzetu huwa wanasherehekea Wiki ya mwanza jijini Tampere Finland.
Mstahiki meya: Mradi wa Mwanza-Tampere, umejipanga kutoka mafunzo mengi sana katika idara nyingi kama vile Madiwani wa kata, watendaji na wenyeviti wa Mtaa, mafunzo ya mazingira kwa ma Afisa afya, walimu na mafunzo ya ushauri na nasaha kwa walimu wa shule.
Mstahiki meya, kupitia ushurikiano huu ndani ya miaka kumi tumepata misaada mingi kama vile gari la kuzimia moto mawili na pia mradi umetoa mafunzo ya compyuta kwa walimu wafanyakazi wa halmashauri wengi na pia mafundisho haya ni ya kuendelea kwa muda wote.   mradi wa mahusiano ya jiji la Mwanza na Tampere umepanga kuwapatia mafunzo juu ya demokrasia na utawala bora,ni dhahiri kuwa mafunzo haya ni ya muhimu sana kwenu katika kuboresha utendaji kazi wenu katika kata na Halmashauri mnazoziongoza.
 Ni vyema kutoa shukrani kwa  wasimamizi wa mradi huu kwa kuandaa mipango mizuri na edelevu kwa kukuza uwezo wa halmashauri yetu katika kuboresha uwezo wa halmashauri yetu ya Mwanza ili kuweza kuwahudumia wakazi wa mwanza kwa ujumla .  .
Ndugu mstahiki meya ,Ni matumaini yangu kuwa mtakuwa wasikivu na  kuyafuatilia kwa makini mafanikio ya mradi huu kwa wadau wote ambao tulikuwa pamoja nao kwenye shughuli za mradi.

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

chanzo:halmashauri ya jiji la mwanza.
Vielezo: , , ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako