Waziri Mkuu Thailand agoma kujiuzulu

Waziri Mkuu wa Thailand amepinga madai ya wapinzani ya kumtaka ajiuzulu.
Yingluck Shinawatra amesema yuko tayari kwa mazungumzo na waandamanaji wanaoipinga serikali yake, lakini ameonya kuwa madai ya kumtaka ajiuzulu ni kinyume cha katiba.

Bi Yingluck amesema polisi hawatatumia nguvu dhidi ya waandamanaji, huku maandamano hayo yakiingia wiki ya pili sasa. Waandamanaji wamelazimisha shule kadha kufungwa pamoja na vyuo na shughuli za biashara.
Lakini kuna waandamanaji wachache zaidi kuliko ilivyokuwa katika siku za karibuni, na mwandishi wa BBC anasema inaonekana waandamanaji hao hawana uwezo wa kuendelea mbele katika kampeni yao ya kutaka kumng'oa madarakani waziri mkuu Yingluck Shinawatra.
Vielezo: , , , , ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako