Katika
maandalizi ya kuuanza mwaka mpya
20I4,
tulikuwa tukiomba na kutakiana heri ili kila mmoja wetu aweze
kuumaliza vizuri mwaka 20I3
kwa amani, bila dhahima yeyote. Pamoja na juhudi zetu katika
kutakiana heri ya mwaka mpya 20I4
na kuhimiza uwajibikaji kikamilifu juu ya usalama wetu wakati
tunaposafiri kwenda kusherehekea sherehe hizo za mwisho wa mwaka kwa
kuruhusu ajari nyingi kutokea barabarani na hivyo kupelekea ndugu na
jamaa zetu wengi kupoteza maisha. Ni ukweli usiopingika kuwa sisi
sote tumekuwa sehemu ya matukio haya ya kusikitisha kwa namna moja
ama nyingine kutowajika kila mtu kwa nafasi yake..
Sisi
kama Watanzania, ili tutambulike na kuheshimika kama taifa kubwa na
lenye nguvu tunahitaji mambo mawili muhimu ambayo ni kuwa na jamii
safi kimaadili, pamoja na uchumi imara. Yote haya hujengwa na
kusitawishwa katika misingi ya utawala bora na uliotukuka.
Utawala
bora ni utawala wa sheria unaolinda jamii dhidi ya matendo ya
kidhalimu ya watawala dhidi ya watawaliwa. Mahakamani kwa mfano,
Hakimu anapaswa kuwa muadilifu na mtiifu kwa haki kuliko chochote,
iwe serikali au mtu yeyote. Kwa maana nyingine ni kwamba kesi
zinazofanana ni lazima ziwe na matokeo yanayofanana. Huo ndio utawala
bora na ambao ndio chemichemi ya jamii inayoheshimu sheria na
muumini wa haki na usawa.
Msingi
wa jamii imara yeyote ile duniani ni haki. Na haki hii, hutekelezwa
na kusimamiwa na serikali ya jamii husika juu ya wanajamii. Serikali
dhaifu katika usimamizi wa haki huzaa rushwa baina ya wasimamizi wa
sheria na wasimamiwa. Huzaa ajari za barabarani. Huzaa uonevu. Na
zaidi ya yote huzaa jamii haramu. Swali, ni namna gani jamii haramu
hutokea?
Nikiwa
chuo kikuu nasoma mwaka wa pili nilibahatika siku moja, kukaa na
wasichana wanne katika meza
moja ya chakula. Tukiwa tunaendelea kula, nilisikiliza maongezi ya
wasichana hao yaliyohusu mahusiano yao ya kimapenzi. Maongezi yao
waliyajengeka
katika mtazamo wa jinsi
gani ilivyo batili kwao kuolewa na
Mwalimu. Katika kujenga hoja walidai mshahara wa mwalimu ni mdogo,
hivyo hautoshi katika kuendesha maisha.
Nikiwa
kama mwanafunzi niliyekuwa nasoma shahada ya ualimu, niligundua kuwa
kama ningelikuwa natafuta mke wa kuoa, basi sikuwa na sifa ya kumuoa
yeyote yule katika lile kundi kwa vile nilikuwa mwalimu mtarajiwa.
Walidai kuwa mwalimu hutoka nyumbani asubuhi na kurudi jioni mikono
mitupu iliyojaa vumbi la chaki. Kwao waliona
kuwa ni heri kuolewa na jambazi kuliko
kuolewa na mwalimu. Nilihamaki ghafla nikaondoka zangu nikihofia
wangeniharibia siku.
Mtazamo
huu si tu kwa wasichana hawa bali kwa jamii nzima. Na mtazamo huo
haramu ulianzishwa na kusitawishwa katika jamii hii hii. Nao ukazaa
matunda haramu. Lakini yana msingi wake, nayo ni kushamiri kwa rushwa
katika jamii na kuwa kama sehemu
ya tamaduni zetu. Hii ndiyo jamii tuliyomo, kwao ni heri nchi
iongozwe na tajiri anayenuka rushwa kuliko
kuongozwa na mtu ambaye ni
maskini, mwadilifu na mtendaji
mzuri.
Sisi
kama taifa, ili tusafishe taswira ya taifa letu mbele ya mataifa
mengine na kunusuru uzao wetu wa kesho, yatupasa tujitazame na
kujitathimini upya tumetoka wapi, tuko wapi na tunaelekea wapi?. Afya
ya maadili inapaswa kujengwa na kulindwa kuanzia kwa viongozi wetu wa
juu kabisa wa taasisi zote,zikiwemo za kisiasa, kiuchumi na za
kijamii. Tuilinde na kuiishi katika
misingi ya haki kuanzia katika jamii,
familia na hatimae mtu mmoja mmoja. Huko ndiko
kujenga jamii bora na yenye maadili. Swali,
ni namna gani tunaweza kujenga uchumi wetu? Na kwa nini serikali
imeshindwa kumea maisha bora(prosperity life) kwa kila mtanzania kama
ilivyoahidi?
Katika
kitabu chao cha “The origins of power, prosperity and Poverty.
Daron Acemoglu na James Robinson” wanaelezea kwa nini baadhi ya
mataifa kwa mfano Botswana, ni moja ya mataifa duniani ambayo uchumi
wake unakuwa haraka zaidi kuliko mataifa mengine kama Congo, Zimbabwe
na Sierra leon, ambayo yamebaki kwenye umasikini wa kutupwa na vita.
Kwa
kutumia mfano wa jiji la Nogoles, Daron na James wanadai kuwa
katikati ya jiji la Nagoles kuna ukuta unaoligawa jiji hili sehemu
mbili, nazo ni Nagoles ya kaskazini na Nagoles ya kusini. Wanadai
ukisimama juu ya ukuta ukatazama kaskazini utaona mji wa Nagoles ya
Arizona. Hii iko katika jimbo la Santa cruz, nchini Marekani. Kipato
cha wakazi wa Arizona ni takribani $30,000 kwa mwaka. Watoto wote
wenye umri wa kusoma wako shule. Watu wazima walio wengi wamehitimu
Vyuo vikuu.
Wana uhakika na matibabu ya bure kutokana na sera ya Rais Barack
Obama(Obama’s health care). Karibu jamii yote ina afya na muda
mrefu wa kuishi (takribani miaka 65). Wanao uhakika wa
huduma nyingine kama Umeme, Mawasiliano,
Usafiri, Sheria na mamraka.
Huenda
kwenye shughuli zao za kila siku bila hofu ya maisha au usalama wao,
na hawaogopi wezi, kutaifishwa wala masharti ya kuwekeza katika
biashara zao. Wanaishi kwa haki na usawa na serikali ndiyo wakala wa
haki na suluhisho la matatizo yao. Na zaidi ya yote, wanaheshimu
demokrasia.
Lakini
katika upande mwingine kusini mwa ukuta, Nagoles Sonara, hatua chache
kutoka kwenye ukuta ni tofauti kabisa. Kipato cha wakazi wa Sonara
kwa mwaka ni robo ya kipato cha wakazi wa Arizona. Watu wazima wengi
hawajahitimu elimu ya chuo kikuu na watoto wengi hawaendi shule. Hofu
imetanda kwa kina mama
mjamzito kutokana na vifo vingi kwa akina mama wajawazito
vinavyosababishwa na huduma duni katika taasisi za afya. Barabara ni
mbovu. Sheria hazimpi raia haki ya kuwekeza. Wanasiasa wa Sonara ni
Waumini wa rushwa na wabadhirifu kupindukia.
Na
mwisho kabisa, Daron na James wanahitimisha kwa kudai kwamba ‘‘
It’s man-made political and economic institutions that underlie
economic success (or lack of it)’’. Kwa tafsiri isiyo rasmi ni
kwamba “ ni taasisi za kisiasa na kiuchumi pekee ndiyo zenye uwezo
wa kukuza au kudumaza uchumi katika nchi husika.
Hivyo
kwa kuzingatia ushawishi wa akina Daron na James sanjari na
marejereo rukuki niliyonayo kutokana na historia ya nchi yangu na
nchi nyingine za kiafrika, napenda nisema kuwa umasikini tulionao
umetokana na utashi wa viongozi wetu. Viongozi wetu hawana nia njema
ya kustawisha taasisi zetu za kiuchumi na za kisiasa.
Taasisi zetu, mfano taasisi za kifedha kama Bank
kuu(BoT) haitekelezi wajibu wake katika misingi ya kizalendo bali
imeachia mianya ya kinyonyaji kutawala katika mfumo wa fedha. Taasisi
hii imekuwa dhaifu mno katika kupambana na udharimu(criminality)
unaokuwa kila kuchapo
ndani ya taasisi hii mhimu katika michakato ya kimaendeleo ya nchi.
Kutokana
na kelele za mataifa mengi tajiri duniani juu ya nchi masikini
kuhifadhi fedha nje ya nchi, haihitaji hata upeo upitao upeo wa
kawaida kubaini kuwa kuna watanzania wengi wametunza fedha zao nje ya
nchi, ziwe zilipatikana kwa njia halali
au haramu. Kutunza fedha nje ya nchi ni matokeo hasi ya taasisi za
kifedha (financial institution) kushindwa kuwahakikishia watu wake
usalama wa mitaji yao kipindi uchumi wa nchi unapotetereka. Hivyo
watu huamua kuwa ni heri
wapeleke fedha zao pahala ambapo patawahakikishia uhai wa mitaji yao
bila kujali madhara yanayoipata nchi yao kutokana na maamzi yao.
Athari tunazozipata hapa ni kudhoofika kwa mifumo yetu ya kifedha
kwani msingi wa fedha ni fedha.
Taasisi
hii pia imeshindwa
kudhibiti mfumko wa riba za juu zinazotozwa na mabenki madogo madogo
kwa wateja wao. Mabenki haya hayawakopeshi wajasiliamali na wafanya
biashara wadogo wadogo kwa misingi ya kizalendo ili kunusuru na
kukuza mitaji yao bali kwa misingi ya kinyonyaji. Haziwawezeshi
wakulima kupata pembejeo wala kuwatafutia na kulinda soko la bidhaa
zinazotokana na viwanda vinavyotengeneza mali ghafi zao.
Hata
hivyo uimara wa taasisi
za kiuchumi hauwezi kuonekana bila kuwepo kwa taasisi imara za
kisiasa(political institutions). Hizi ndizo zinazopanga sera na
mikakati ya kimaendeleo na kuhakikisha zinasimamiwa kwa misingi ya
ilani ya chama kilichopo madarakani.
Bahati
mbaya sana nchini Tanzania na Barani Afrika kwa ujumla, nguvu za
kisiasa hutafsiriwa kama dhana ya mafanikio na maisha bora kwa
mwanasiasa husika. Siyo tu kwa anayeshika madaraka hayo bali pia kwa
familia yake, uzao wake na ikiwezekana hata eneo alilozaliwa. Mtazamo
huu umejengwa katika msingi wa ubadhirifu, unyonyaji, ufisadi na
kutowajibika.
Katika
ripoti yake ya transnational crime in
the developing world, Jeremy Haken 2024
anadai nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania hupoteza dolar trillion
moja kwa mwaka kupitia njia haramu za mifumo ya kifedha(illicit
finacial flow, IFF) ambazo
hutokea katika nyanja tatu nazo ni pamoja na rushwa kupitia kwa
wanasiasa na watumishi wa umma(political
corruption), nayo huchukua 3%. Pili uharamia wa
kimataifa(international crime), yaani wizi utokanao na biashara
haramu kama madawa ya kulevya, utoroshaji wa fedha nje ya nchi(money
laundering), biashara za watu, nyara za serikali n.k (nao ni
takribani 35%). Wizi wa tatu ni ule unaotokana na ukusanyaji duni
wa mapato(commercial transactional) nao ni
ukwepaji wa kulipa mapato stahiki, ambao ndiyo umeenea kila kona ya
nchi yetu. Huu huchua 62% iliyobaki. Hii huhusisha ukadiriaji wa juu
kwa bidhaa zinazoingizwa nchini na ukadiriaji wa chini kwa bidhaa
zinazotoka nje ya nchi. Bila ya shaka Tanzania ni moja ya Wahanga na
wathirika wa mfumo huu dharimu na hatari kwa ustawi wa uchumi na
jamii kwa ujumla.
Ili
kuzishinda changamoto hizi na kuhakikisha uchumi wetu unakua na kumea
maisha bora kwa kila mtanzania, hatuhitaji kiongozi mwenye sifa za
urais pekee, bali twapaswa kutafuta na kupata kiongozi mwenye sifa
zaidi ya uongozi. Kiongozi atakayetutoa tulipopotekea
na kutupeleka tunapotaka kwenda. Kiongozi atakayehakikisha taasisi za
kiuchumi na kisiasa zinafanya kazi kwa pamoja katika kuhakikisha
maendeleo ya nchi yanafikiwa.
0 Maoni Kuhusu Habari Hii