WAANDISHI WANA DHAMIRA YAKWENDA CHINA KUJIONEA HALI YA WATANZANIA WALIOSHIKWA NA DAWA ZA KULEVYA


MWENYE KITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI  WA KUPIGA VITA MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA NA UHALIFU TANZANIA {OJADACT) Ndugu Edwini Soko 

Kwa  mujibu  wa  Mwenyekiti wa OJADACT   Bwana  Edwin Soko,  Chama  Cha Waandishi wa  Habari  wa Kupiga  Vita  Dawa  za Kulevya  na Uhalifu Tanzania, kina  mpango wa  kupeleka  waandishi  wake  Nchini China  ili kujionea   sakata  la watanzania  wanaotuhumiwa  kujihusisha  na dawa za kulevya.

Kwa mujibu wa Soko, hali    ni mbaya  kwa watanzania, kwani  wengi  wanashikiliwa  kwenye  magereza  Chini China  kwa kukutwa  na dawa za kulevya, kimsingi  amesema  kuwa hakuna mawasiliano ya  karibu  ya kujua  idadi  ya watanzania  walioshikiliwa Nchini  humo.

Soko  amesema kuwa  pia  kuna malalamiko  toka  kwa baadhi ya  watanzania  wanaoishi  Nchini  China  kunyanyaswa  kwa kuhisiwa  kuwa ni watu  hatari  wa madawa ya  kulevya.

ODAJACT kimeanza mazungumzo  na  ubalozi  wa Tanzania  Nchini  China kupitia kwa mmoja wa maafisa wake  Bwana Edmund  Kitokezi  juu  ya  kuanza mipango  ya kuwapeleka  waandishi wa habari  Nchini humo kujionea  hali  halisi    ili waweze kuandaa  ripoti maalumu  ambayo  itaeleza   ukweli  juu  ya  watanzania  wanaoshikiliwa nchini  humo  kwa tuhuma  za dawa  za kulevya.

Kwa sasa  OJADACT   zote zilizoelekekwa na ubalozi  ili kufanikisha  safari  hiyo.

Wito. Dawa  za kulevya  ni  hatari   kwa  jamii, 
Vielezo: , , , ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako