Waandalizi wa maandamano waonywa Burundi

Burundi
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ameonya kuwaadhibu vikali wote wanaopanga maandamano ya raia dhidi yake.
Kwenye hotuba aliyowasilisha kupitia kituo cha radio ya serikali, siku ya Leba Dei, Kiongozi huyo amesema serikali itaweka vikwazo vikali dhidi ya wale aliowataja kama waasi.
Aidha amesema jopo maalum la mahakama limeundwa kuchunguza maandamano ambayo yameingia siku ya sita sasa.
Waandamanaji wanapinga hatua ya Rais huyo kuwania muhula wa tatu.
chanzo bbc
Vielezo: ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako