Ban Ki-Moon aanza ziara yake DRC



Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki Moon anazuru eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasa ya Congo ambako kumekuwa na mapigano ya siku tatu kati ya vikosi vya serikali na waasi wa m23.
Ban anatarajiwa kukutana na wanachama wa kikosi kipya cha umoja wa Mataifa ambacho kimeundwa ili kukabiliana na makundi ya waasi katika eneo la Maziwa Makuu.

Ziara ya bwana Ban inakuja siku moja baada ya benki ya dunia kuahidi msaada wa dola bilioni moja kusaidia kuimarisha maendeleo katika eneo hilo, lakini pesa hizo zitategemea ikiwa pande mbilizn zinazozozana zitatii mkataba wa amani utakapoafikiwa.
Ziara hiyo inakuja siku moja
Eneo la Mashariki mwa DRC, nlimenaswa katika miaka ishirini ya vita kati ya wanajeshi wa makundi ya waasi wanaaminiwa kuungwa mkono na Rwanda pamoja na waliokuwa washirika wa mauaji ya Kimbari nchini Rwanda mwaka 1994.
Kuna matarajio mengi kuwa kikosi hicho cha UN kitaleta utulivu katika eneo hilo lenmye utajiri mkubwa wa madini.
Mapigano yanaendelea kati ya majeshi ya serikali na waasi wa M23 katika mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mapigano hayo yanatokea wakati katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon na mkuu wa benki ya Dunia Jim Yong Kim wakizuru taifa hilo.
Mashambulio yamezidi katika makaazi ya raia.
Wapiganaji hao wa M23 walikuwa wameahidi kusitisha mapigano wakati wa ziara hiyo ya Ban Ki Moon

chanzo bbc
Vielezo: , , , ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako