Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema nchini Tanzania,
Freeman Mbowe, amevituhumu vyombo vya dola kuwa, vinawafahamu watu
waliohusika na mlipuko wa bomu uliotokea juzi katika viwanja vya Soweto
kwenye mkutano wa chama hicho. Mbowe, amesema tukio hilo ni la kisiasa
na lilipopangwa awali. Amesema wamegundua risasi za bunduki aina ya SMG
na bastola zilitumika mara baada ya mlipuko huo jambo linalozusha hofu
na kuhatarisha demokrasia ya vyama vingi nchini tanzania. Kwa upande
wake Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Said Mwema ameunda timu
itakayoongozwa na makamishna wawili, kwenda mkoani Arusha kuongeza nguvu
ya uchunguzi wa tukio hilo. Mbowe amesema ni bora serikali itangaze
kuachana na mfumo wa vyama vingi kuliko kuruhusu mauaji na vurugu katika
mikutano ya vyama vya upinzani vinavyoonekana kutoa wakati mgumu kwa
watawala. Amesisitiza kuwa, uchunguzi wa awali katika eneo la tukio
umebaini kuwa bomu lililolipuliwa ni la kiwandani na si la kutengenezwa kwa mikono
Afrika,
afrika mashariki,
Tanzania,
Ushirikiano Kimataifa
»
Mbowe: Serikali inawafahamu wahusika wa bomu
Mbowe: Serikali inawafahamu wahusika wa bomu
Imewekwa na tmgtz.blogspot.com/
Tar: 12:54 AM
katika
Afrika,
afrika mashariki,
Tanzania,
Ushirikiano Kimataifa
|
0
Maoni Kuhusu Habari Hii

0 Maoni Kuhusu Habari Hii