Benki ya Exim ya Tanzania imefungua huduma mpya ya Dirisha la Biashara la Tanzania-China, ili kukuza biashara baina ya nchi hizo.
Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa
Benki ya Exim, Anthony Grant jana ilisema huduma hiyo mpya itawawezesha
wateja kupata njia nzuri ya kufanya malipo ya bidhaa zinazoingia na
kutoka kwa kutumia fedha ya China.
Grant alisema benki yake tayari imeingia ubia na
Benki ya HSBC iliyopo mjini Hongkong na kuongeza kuwa, huduma hiyo mpya
itatoa viwango vya riba vya ushindani kwa wafanyabiashara wa nchi hizo.
“Kupitia huduma hii mpya, wafanyabiashara wa Tanzania na China watapata nafuu ya kutuma na kupokea fedha kwa urahisi.”
Pia, Grant alisema benki yake imeamua kufungua
huduma hiyo mpya kutokana na kukua kwa biashara kati ya Tanzania na
China kwa miaka ya karibuni.
Kwa mujibu wa takwimu kutoka Benki Kuu ya Tanzania
(BoT), bidhaa zinazosafirisha kwenda China zimeongezeka kutoka dola 101
bilioni mwaka 2005 mpaka dola 908 bilioni kwa mwaka 2010.
Chanzo: Mwananchi Tovuti
Chanzo: Mwananchi Tovuti
0 Maoni Kuhusu Habari Hii