Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ametangaza hatua ya kuwafukuza mabalozi wa Marekani nchini, ikiwa pamoja na mwakilishi mkuu Kelly Keiderling. Wengine ni watumishi wawili wa ubalozini.
Wanadiplomasia hao wamepewa muda wa saa 48 kuondoka nchini Venezuela. Rais wa Venezuela amesema kuwa anao ushahidi wa shughuli za kuvunja sheria za mabalozi hao. Hata hivyo Rais Maduro hakutoa maelezo zaidi juu ya shughuli za Wamarekani hao licha ya kufahamisha kuwa walikutana na viongozi wa upinzani na wa vyama vya wafanyakazi katika jimbo la kusini magharibi mwa Venezuela.
Wanadiplomasia hao wamepewa muda wa saa 48 kuondoka nchini Venezuela. Rais wa Venezuela amesema kuwa anao ushahidi wa shughuli za kuvunja sheria za mabalozi hao. Hata hivyo Rais Maduro hakutoa maelezo zaidi juu ya shughuli za Wamarekani hao licha ya kufahamisha kuwa walikutana na viongozi wa upinzani na wa vyama vya wafanyakazi katika jimbo la kusini magharibi mwa Venezuela.
0 Maoni Kuhusu Habari Hii