Watu 134 Mbaroni kwa Ukatili na Unyanyasi wa kijinsia huko Tanzania

 Habari na ,Mwandishi wetu. Simba Kabonga... mwanza

Mwanza, 25,Novemba 2013: mkuu wa polisi mkoa wa mwanza kamanda Ernest Mangu  , amezindua rasmi siku 16 za  kupambana na ukatili wa jinsia . Akipokea maandamano ya wadau na vikundi mbali mbali vya kupambana na ukatili wa jinsia kutoka mikoa mbali mbali kanda ya ziwa
. Akiongea katika uzinduzi huo uliofanyika katika viwanja vya mabatini line polisi, katika hotuba yake kamanda Mangu alivipongeza na kuvishukuru vikundi  hivyo vya kijinsia na kusema kuwa kazi hizo za kuzuia unyanyasaji na ukatili  wa kijinsia mara ya kwanza shughuli hizo  zilifanywa na jeshi la polisi pekee.
  Katika kupambana na unyanyasaji wa kijinsia jeshi la polisi limeaanzisha Dawati maalumu kwa kushirikiana na vikundi shirikishi vya kupambana na ukatili wa kijinsia . Dawati linafanya kazi yake vizuri na kwa ufanisi mkubwa kuhakikisha linaweza kutokomeza kabisa vitendo hivyo. 
Alisema jeshi la polisi mpaka sasa limeshikilia na kuwafikisha mahakamani watu 134 katika mkoa mwanza akitoa takwimu hizo amezitaja wilaya zinazoongoza kwa ukatili   pamoja na mauaji ya vikongwe.wilaya  za kwimba misungwi na magu.


Uzinduzi huo ulihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa mkoa wa mwanza wakiwemo madiwani,viongozi wa kidini watendaji wa kata, wenyeviti serkali za mitaa na viongozi kutoka taasisi mbali mbali za kijinsia.

Akizungumza katika uzinduzi huo  Mkurugenzi wa taasisi ya KIVULINI Ndugu Ramadhani Masele alisema taasisi yake inajitaidi sana kumbana na unyanyasaji mkubwa kwa kuzipeleka  kesi mahakamani lakini wanakutana sana na vikwazo kutoka katika familia haswa kesi zinapokuwa katika hatua ya hukumu .

Maandamano hayo yalifanyika siku ya jumatatu yakianzia katika bustani za Mahatma Ghandhi na kupitia barabara za uhuru na nyerere Road
Vielezo: , , , , ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako