Watu 11 wauawa katika mashambulizi mjini Baghdad



Polisi nchini Iraq wamesema mashambulizi matatu ya mabomu yaliyotokea mjini Baghdad yamesababisha vifo vya watu 11 na wengine 45 kujeruhiwa. Mashambulizi hayo ya mabomu yaliyotegwa ndani ya magari na kando ya barabara yalitokea katika masoko mawili na mtaa wenye maduka ulio katikati ya Baghdad. Takwimu zinaonesha kuwa mwaka jana watu 8,868 waliuawa katika mashambulizi ya kigaidi na mapambano ya kimabavu yaliyotokea katika sehemu mbalimbali nchini Iraq.
Vielezo: , ,

Swahili Zone

Tovuti huru habarishi (blogu) inayoendeshwa kiueledi yenye lengo mahususi la kuifikishia jamii habari, makala na matukio wakati muafaka inapowezekana kufanya hivyo!

0 Maoni Kuhusu Habari Hii

Andika Maoni Yako